Tanzania
imependa kwa nafasi 12 kwenye orodha ya viwango vya ubora ya Shirikisho
la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) iliyotolewa leo (Julai 4 mwaka
huu) na shirikisho hilo.
Kwa
viwango vya Juni mwaka huu, Tanzania (Taifa Stars) ambayo timu yake
inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilikuwa namba 139 hivi sasa
imefika nafasi ya 127 ikiwa na pointi 253 kulinganisha na 214 za Juni
mwaka huu.
Ivory
Coast inayoshika nafasi ya 16 duniani bado inaongoza kwa upande wa
Afrika ikiwa na pointi 939. Timu hiyo ilikuwa katika nafasi hiyo hiyo
kwa viwango vilivyotolewa Juni 6 mwaka huu. Hispania ambao ni mabingwa
wa Ulaya na Dunia ndiyo wanaoendelea kuongoza kwa kukamata nafasi ya
kwanza wakiwa na pointi 1,691.
No comments:
Post a Comment