MDAU POPOTE ULIPO TUMA PICHA NA HABARI KWA E-mail:  antonysiame74@yahoo.com

Wednesday, November 6, 2013

SIMBA YAIADHIBU ASHANTI UNITED TAIFA


Ramadhani, Singano (Mess), Amis Tambwe, Betram Mwomeki waing'arisha Simba Taifa baada ya kuitandika Ashanti United bao 4-2 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam leo

Wakati huohuo lile pambano kali la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya wana Mbeycity na wanalambalamba, Azam FC linalosubiriwa kwa hamu litapigwa  kwenye Uwanja wa Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam

Tayari mashabiki wa Mbeyacity kutoka jijini Mbeya wamekwishatinga hapa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuishangilia timu yao inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu Tazania Bara ikiwa nyuma ya Azam FC watakayopambambana nayo kwa tofauti ya mabao ya kufunga.

Nayo mabingwa wa Tanzania Bara, Dar Young Afrian nao kesho watajitupa uwanjani kumenyana na timu ya Jkt Oljoro ya jijini Arusha katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, Yanga inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara
 

No comments:

Post a Comment