MDAU POPOTE ULIPO TUMA PICHA NA HABARI KWA E-mail:  antonysiame74@yahoo.com

Friday, March 7, 2014

UJUMBE WA SIKU YA WANAWAKE DUNINANI

Hii ni Siku ya Wanawake Duniani, tunasisitiza umuhimu wa usawa wa kijinsia kwa wanawake na wasichana sio tu kwa sababu ni suala la haki na haki za msingi za binadamu, lakini kwa sababu maendeleo katika maeneo mengine mengi yanategemea hili.


Nchi ambazo kuna usawa zaidi wa kijinsia na zina ukuaji mzuri wa kiuchumi. Makampuni yenye viongozi wengi wa kike yanafanya vizuri. Makubaliano ya amani ambayo yanahusisha wanawake yanadumu kwa muda mrefu zaidi. Mabunge yenye wanawake wengi hutunga sheria nyingi zaidi juu ya masuala muhimu ya kijamii kama vile afya, elimu, kupambana na ubaguzi na msaada wa watoto.

Ushahidi uko wazi: usawa kwa wanawake ni maendeleo kwa wote.

Suala la ukweli ni muhimu tunapofanya kazi kuharakisha maendeleo kuelekea kwenye Malengo ya Maendeleo ya Milenia kwa tarehe ya mwisho ya mwaka ujao na kutengeneza ajenda kwa miaka inayofuata ya baada ya 2015.

Mafanikio muhimu yamepatikana katika upatikanaji wa elimu ya msingi kwa ajili ya wasichana na uwakilishi wa kisiasa na wanawake. Lakini mafanikio bado ni madogo na yanatofautiana.

Msichana anayezaliwa leo bado anakabiliwa na kukosekana kwa usawa na ubaguzi, bila kujali mama yake anaishi wapi. Tuna wajibu wa kuhakikisha anapata haki yake ya kuishi mazingira yasiyo vurugu ambayo huathiri mwanamke mmoja katika wanawake watatu duniani; haki ya kupata mshahara sawa na kwa kazi sawa; kuwa huru na ubaguzi unaozuia haki yake ya kushiriki katika uchumi; kuwa na haki ya usawa katika kusemea maamuzi yanayoathiri maisha yake; haki ya kuamua kama anataka na lini atakuwa na watoto, na ni wangapi.

Mimi nina ujumbe kwa kila msichana aliyezaliwa leo, na kwa kila mwanamke na msichana aliye juu ya sayari: kutambua haki za binadamu na usawa si ndoto, ni wajibu wa serikali, Umoja wa Mataifa na kila binadamu.

Mimi pia nina ujumbe kwa ajili ya wanaume wenzangu na wavulana: timiza wajibu wako. Sisi sote tunafaidika wakati wanawake na wasichana - mama yako, dada, marafiki na wafanyakazi wenzako – wanapewa nafasi ya kufikia uwezo wao.

Kwa pamoja, basi, tufanye kazi kufikia haki za wanawake, uwezeshaji na usawa wa kijinsia wakati tukijitahidi kuondoa umaskini na kukuza maendeleo endelevu. Usawa kwa wanawake ni maendeleo kwa wote!







No comments:

Post a Comment