Mchezaji wa Simba, Haruna Moshi (BOBAN) aliyeshikwa mkono akiwa mwenye huzuni baada ya kupata taarifa za msiba
Boban akiwa ameinama
Boban katikati akiwa ameshikiliwa
Mchezaji wa Kimataifa wa timu ya Simba, Kiungo Patrick Mafisango amefariki Dunia kwa ajali ya gari eneo la Tazara Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo, katika picha hii alikuwa akishangilia baada ya kuifungia moja ya goli dhidi ya Yanga katika mchezo wa mwisho wa ligi Kuu uliochezwa katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mei 6 ambapo Simba ililishida goli 5-0. Mungu ailaze roho ya marehemu Peponi Amina. Poleni wanamichezo wote ikiwa ni pamoja na wapenzi wa timu ya Simba na kwa uongozi wa Klabu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi
No comments:
Post a Comment