MDAU POPOTE ULIPO TUMA PICHA NA HABARI KWA E-mail:  antonysiame74@yahoo.com

Monday, February 11, 2013

Tanzania yashinda maajabu Saba ya Afrika


HATIMAYE vivutio vitatu vya kitalii vya nchini Tanzania vimefanikiwa kuingiza katika maajabu Saba ya Bara la Afrika.
Vivutio vya kitalii vilivyoshinda na kuingia maajabu Saba ni Mlima Kilimanjaro, Ngorongoro Creater na mbuga ya wanyama ya Serengeti.
Sherehe za kutangaza vivutio vilivyoshinda ilifanyika jana jijini Arusha na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ndiye aliyekuwa mgeni rasmi ambapo wageni mbalimbali kutoka nje na ndani ya nchi walihudhuria.
Akizungumza mara baada ya kutangazwa kwa maajabu hayo Pinda aliwataka Watanzania kutumia fursa hiyo kuvitangaza na kuvienzi vivutio hivyo ili vizipoteze sifa yake.
“ Changamoto iliyopo mbele yetu ni kuhakikisha vivutio hivi vilivyoshinda na vingine tuna vilinda na kuvitunza ili visiendelee kupoteza sifa,” alisema Pinda.
Akizungumzia maajabu ya Hifadhi ya Serengeti Pinda alisema, hifadhi imefanikiwa kuingia na kushinda katika maajabu Saba ya Afrika kutokana na upekee wake wa kuwa na histori ya aina yake.
Aliitaja historia hiyo kuwa ni pamoja na kuwa na sifa ya kipekee inayotambulika kama sehemu ya urithi wa dunia iliyopo chini ya UNESCO, ikiwa pia na wanyama aina ya Pundamilia takribabni 200,000 na Swala  takriban 300,000.
Kwa upande wa Mlima Kilimanjaro Pinda alisema kivutio hicho kimefanikiwa kushinda kutokana na kuwa ndio Mlima mrefu pekee barani Afrika ukiwa pia ni sehemu ya urithi wa dunia inayotambuliwa na UNESCO.
Pinda aliendelea kubainisha kwamba kwa upande wa Ngorongoro pamoja na kuwa ipo ndani ya sehemu ya urithi wa dunia inayotambuliwa na UNESCO pia ndio sehemu pekee duniani ambayo wanyama wa porini wanaishi kwa kuchanganyika na binadamu na wanyama wa kufungwa.
Katika hatua hiyo Pinda aliwashukuru Watanzania na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kwa kuvipigia kura vivutio hivyo na hatimaye kuweza kufanikiwa kuingia katika maajabu Saba ya dunia.
Kwa upande wake Rais wa Taasisi ya Maajabu Saba ya Dunia Dk. Phillip Imler akitangaza vivutio vingine vilivyoshinda baada ya kupigiwa kura ambapo alivitaja kuwa ni pamoja na Mto Nile, Red See Reefs, Sahara Desert na Olevango Delter iliyopo nchini Botswana.

Pamoja na wageni kutoka nje ya nchi baadhi ya wageni wengine waliohudhuria sherehe hizo ni pamoja na wabunge, wakuu wa wilaya na watendaji na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii nchini.



No comments:

Post a Comment