Spika wa Bunge Anne Makinda akiwafarija ndugu wa Marehemu Regia Mtema aliyekuwa Mbunge wa Viti maalum mkoani Morogoro kupitia CHADEMA aliyefariki kwa ajali ya gari eneo la Ruvu Darajani mkoani Pwani siku ya Jumamosi saa tano akitoka Chalinze. Mwili wa marehemu unatarajia kusafirishwa kwenda Ifakara kwa mazishi yatakayofanyika jumatano. Kabla ya kusafirishwa Mwili utaagwa kiserikali katika Ukumbi wa Karimjee siku ya Jumanne
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akitia saini kitabu cha maombolezo
Rais Jakaya kikwete akitia saini kitabu cha maombolezo
Ndugu wa Marehemu Regia wakiwa wenye majonzi
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (katikati) Mbunge wa Msoma Mjini, Vicent Nyerere (kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chama hicho, John Heche wakiwa kwenye Msiba
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika akihojiwa na waandishi wa habari kwenye msiba kuhusiana na msiba huo
Spika Anne Makinda akihojiwa na waandishi wa habari
No comments:
Post a Comment