MDAU POPOTE ULIPO TUMA PICHA NA HABARI KWA E-mail:  antonysiame74@yahoo.com

Thursday, February 28, 2013

MKUTANO MKUU WA CHAMA CHA WAANDISHI WA hABARI ZA MAZINGIRA (JET)


Chama cha waandishi wa habari za Mazingiara (Jet) kitafanya Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama hicho jijini Dar es Salaam saa tatu kamili asubuhi juu ya alama. Usajili wa wajumbe wa mkutano utaanza saa mbili kamili asubuhi.  Tafadhali tuwahi ili shughuli ianze mapema na tumalize mapema.

 Mtakumbuka kuwa nimewasiliana nanyi mara tatu nikiwakumbusha wote kuthibitisha kuhudhuria mkutano ili sekretariati ya JET iweze kuandaa yale ambayo wajumbe wanapaswa kupata.  Idadi ya waliothibisha ni 44, hivyo sekretariati imejiandaa kwa ajili ya kuhudumia idadi hiyo.

Wale wanachama hai ambao hawakuthibitisha kuhudhuria mkutano
wanakaribishwa, lakini stahili nyingine hazitawahusu, kwa maana ya kulipwa nauli posho na kadhalika.
Naomba kuwasilisha.

MKUTANO MKUU WA MWAKA 2013

WALIOTHIBITISHA KUUHUDHURIA
NO.
JINA
MKOA
NAMBA YA SIMU
1.
Felix              Endrew
D’Salaam

2.
Dr. Ellen        Ockedion
D’Salaam
0784 401884
3.
Chrysostom Rweyemamu
0713  329005
4.
Gerald            Kitabu
0713  612698
5.
Johnson         Mbwambo
0754  564916
6.
Harieth           Kiwale
D’Salaam

7.
Ludger            Kasumuni
D’Salaam
0754 458911
8.
Travena        Maimu
D’Salaam

9.
Upendo        Mwinchande
D’Salaam
0652 487457
10
Janet             Shekunde
D’salaam

11
Sekela           Mwambuli
D’Salaam
0758 405474
12
Aisha              Dachi
D’Salaam
0754 467133
13
Judica             Losai
0713357713
14
Deodatus       Mfugale
0754 275170
15
Sidi                  Mgumia
0714 327572
16
Endrew         Chale
0719 076379
17.
Josefu            Lino
0712 431537
18.
Antony          Siame
0713 403248
19.
Stella             Barozi
0718 194414
20.
Christina       Mokimilya
0715 686705
21.
Simon          Nyalobi
0785 345489
22.
Lucy             Ogutu
D’Salaam
0713 540994
23.
John             Chikomo
D’Salaam
0754 263965
24.
Mwanaharusi  Pongwa
D’Salaam
0715 444792
25.
Felix              Mwakyembe
Mbeya
0713 290487
26.
Brandy         Nelson
Mbeya
0754 011770
27.
Jumbe           Ismail
Singida
0754 080740
28.
Ali                    Hamad
Pemba
0777 458523
29.
Zainab        Mwatawala
Morogoro
0655 423456
30.
Salome       Kitomari
Moshi
0754 080740
31.
Ileje Env Conservation group
Mbeya

32.
Albano       Midelo
Songea
0784 765917
33.
Ashton       Balaigwa
Morogoro
0713 811110
34.
Haji             Mohamed
Pemba
0777 870191
35.
Joseph       Malembeka
Morogoro
0655 824151
36.
Fitina          Haule
Morogoro
0754 654678
37.
Henry         Mwakifuna
Ifakara, Morogoro
0764 516666
38.
Vedasto     Msungu
Morogoro
0713 640700
39.
Nathaniel   Limu
Singida
0755 417789
40.
Editha            Karlo
Kigoma
0752 202783
41.
Anthony      Kayanda
Kigoma

42.
Alisante      John
Singida

43.
Esther         Macha
Mbeya
0753  804343
44.
Jane             Sume
Arusha




CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI ZA MAZINGIRA TANZANIA (JET)

(RIPOTI YA UTENDAJI FEBRUARI 25, 20012 – MACHI 2, 2013)


1.0           Muhtasari
Kwa kipindi cha mwaka mzima tangu mkutano mkuu ufanyike mwaka jana Februari 25 (2013), JET imetekeleza mambo kadhaa yakihusisha uchapishaji wa gazeti la Kasuku,  kuhamasisha waandishi kujiunga na JET, kutathmini uharibifu wa mazingira katika sehemu mbalimbali nchini zikihusisha Bonde la Mto Kilombero ambalo limeharibiwa sana na wafugaji, Mlima Kilimanjaro ambao uasili wake sehemu zenye misitu umeharibiwa mno pia; tumetembelea pia mikoa ya Lindi, Mtwara na Pwani ambako misitu imefyekwa sana bila utaratibu, na uvuvi haramu kuendelea kwa kasi katika mikoa hii.

Aidha, tumetembelewa na wageni mbalimbali kutoka  hapa nchini na nje ya nchi, washirika mbalimbali wamekuja kwenye ofisi za JET kuona namna ambavyo tunaweza kufanya kazi pamoja wakiwamo Mama Misitu Campaign (MMC) na Revenue Watch Insitute inayojihusisha na uandishi wa masuala ya gesi, mafuta na madini yenye makao makuu jijini New York, Marekani na ofisi zake za kanda zikiwa jijini Accra, Ghana; na hivi karibuni Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeomba JET ifanye kazi kwa karibu nalo, hasa katika sehemu za vyanzo vya maji ambavyo hatimaye hupeleka maji katika mitambo ya kufua umeme huko Kidatu (Morogoro)  na Mtera (Iringa).

Pia katika kipindi hiki hiki, JET imeweza kutengeneza documentary mbalimbali za mazingira, imeshiriki katika kutoa maoni kuhusu Katiba mpya na tumeweza kuhamia katika ofisi mpya zilizo Tegeta, Dar es Salaam (off Bagamoyo Road, Barabara ya Chanika mara baada ya kupita Kibo Commercial Complex kama unaelekea Bagamoyo). Kuhama huku kulitokana na mwenye jengo tulikokuwa katikati ya jiji, Mnazi Mmoja, kututaka tuondoke.     

2.0           Kwa ufupi, katika kipindi cha Februari 25, 20012 hadi leo Machi 2 mwaka huu (2013), JET imejitahidi kwa uwezo wake kutekeleza majukumu yaliyotajwa hapa chini:

·        Kusimamia utekelezaji wa miradi mipya na ya zamani.
·        Kuandaa  safari za kikazi mikoani (field trips) kwa waandishi wa habari
·        Kuandika miradi mipya na kuiwasilisha kwa wafadhili
·        Kuandaa na kuchapisha gazeti la Kasuku/JET News
·        Kuandaa rasimu ya katiba mpya ya JET
·        Kushirikiana na vyama vingine vya mazingira ndani na nje ya nchi
·        Kuhamasisha waandishi zaidi kujiunga na JET

3.0 Miradi
3.1 Mradi wa Fredskorpset ambao ni wa kubadilishana vijana wasiozidi miaka 35 kwa nchi za Tanzania, Uganda, Kenya na Ethiopia uliendelea vizuri mwaka jana kwa mwaka wa 10 mfululizo, na unaendelea tena kwa mara ya mwisho mwaka huu.
Vijana wetu, Jamilah Khaji na Sidi Mgumia walifanya vizuri huko Kenya na Uganda; na vijana waliopokewa nasi pia walifanya vizuri. Adamu Mussa kutoka Uganda alifanya kazi kwenye gazeti la The Citizen na Nicholas Begisen kutoka Kenya, ambaye alianzia  kwenye gazeti la The African, alimalizia shughuli zake kwenye gazeti la The Guardian.
Kama ilivyo taratibu za mradi huu, kuanzia Julai 17 hadi 21 mwaka jana (2012) kulifanyika mikutano ya Review na Planning kwa ajili ya maandalizi ya mradi wa mwaka 2012/2013. Mkutano huo ulifanyika Kampala, Uganda.
Kwenye mkutano huo, Mkurugenzi wa FK Africa Regional Office, Fikre Haile Meskel, alitoa maelezo ya mabadiliko ndani ya FK Oslo. Mabadiliko hayo ni pamoja na kubadilika kwa sera, mwonekano, bajeti, na ukomo wa ubadilishanaji wa wafanyakazi.
 Alieleza kuwa mabadiliko hayo ya kiutendaji na kimfumo si tu yamebadilika huko Norway, bali pia ni kwa wote wanaohusika katika mradi huu wa kubadilishana washiriki (partners).
Alisema kwamba tayari mitandao (networks) miwili, yaani AMPCAN pamoja na MEDIA WOMEN zimekwisha kufikia ukomo wa kushiriki, na mtandao (network) unaofuata kufikia ukomo ni ya Environmental Journalists ambao sisi  JET ndio tunauongoza. Kwamba sasa tumepewa mwaka wa mwisho wa kushiriki katika mradi huu.
Maandalizi ya mradi huu kwa mwaka 2012/2013 yalienda vizuri na tunaendelea vizuri. Tayari tumepokea vijana wawili, mmoja kutoka EEJA, Ethiopia na mwingine kutoka VCDO, Kenya. Nasi tumepeleka vijana wetu wawili, mmoja RUDMEC nchini Uganda na mwingine VCDO nchini Kenya.
Mafunzo ya wiki mbili yajulikanayo kama FK PREPARATORY COURSE kwa vijana waliochaguliwa kushiriki kwenye mradi huu yalifanyika jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini katika wiki ya kwanza ya Novemba mwaka jana (2012). Vijana waliokwenda kwenye mkutano huo walitoka Tanzania, Kenya, Uganda na Ethiopia.
Katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya JET iliyokaa hivi karibuni ilijadili na kubungua bongo (brainstorm) kuhusu mradi huu wa Fredskorpset ambao unakaribia kufika ukingoni, yaani mwaka huu.
Mradi huu kwa muda mrefu ndio ulikuwa unabeba shughuli za JET kwa asilimia 80, hivyo kulikuwa na ulazima wa kujadili na kubungua bongo kuhusu njia nyingine mbadala za kuhimili shughuli za JET baada ya Fredskorpset kufikia mwisho.
Baadaye ilibainika kuwa JET inahitaji miradi mikubwa minne ili kuziba pengo litakaloachwa na Fredskorpset. Aidha, Kamati ya Utendaji ilikubaliana kufuatilia plan B ya Fredskorpset, kwamba taasisi moja moja inaweza kuomba yenyewe ufadhili wa Fredskorpset kama inaona ina hoja, na ikizingatiwa kwamba JET inaweza kufanya hivyo kwa sababu suala la mazingira, hasa mabadiliko ya tabianchi (climate change), ni muhimu na nyeti kwa sasa duniani kote.
3.2 Mradi wa Mama Misitu (Mama Misitu Campaign – MMC): Mradi wa Mama Misitu ni wa miaka mitano – na umeanza kutekelezwa hivi karibuni katika wilaya za Kilwa, Kisarawe na Kibaha.  JET ni mmoja wa  washiriki (partners) kadhaa wanaotekeleza mradi huu, sisi JET tukitekeleza mradi huu katika eneo la makala, redio/TV programu na uchapishaji wa gazeti la Kasuku. Kabla ya kupewa mradi huu, sharti la wafadhili lilikuwa kuwa ni lazima mratibu wa mradi (project co-ordinator) na mhasibu wa mradi waajiriwe.
Hilo limefanyika, na MMC waliweza kufanya ziara mbili katika ofisi za JET, moja ikiwa ni wao kujitambulisha kwetu sisi kama moja ya asasi zitakazotekeleza mradi.
Ziara yao ya pili ilikuwa ni kuangalia uwezo wetu kiutendaji na kifedha (Organisation Capacity na Financial Capacity).  Uzinduzi wa mradi huu ulifanyika Julai 31 mwaka jana (2012).

3.3 Mradi wa “Advocacy and Awareness Raising Campaign to Policy and Decision makers on the Effects of Dynamite Fishing”
Mradi huu ambao umefadhiliwa na The Foundation for Civil Society (FCS) ni mradi wa miaka mitatu kuhusu eneo la utawala bora na uwajibikaji.
Katika kipindi cha Aprili hadi Julai mwaka jana, JET iliweza kutembelea vijiji vya mkoa wa Mtwara na kufanya tathmini, kuongea na wadau WWF-Mtwara, BMU Msanga Mkuu, Mnazi Bay Marine Park, Polisi mkoa na Msajili wa Mahakama Kuu kanda ya Mtwara ili kutathmini mwenendo wa uvuvi na kuandaa vipindi vya redio na kuandika makala.
Mbali na tathmini hiyo, tumeendelea kutoa makala mbalimbali juu ya hali halisi ya uvuvi wa kutumia baruti, kuperemba (monitor) jitihada zinazofanywa na wadau mbalimbali, changamoto, mafanikio, sheria ya uvuvi ya mwaka 2003 na mambo ya kufanya ili kurekebisha hali iliyopo.  
Utekelezaji wa mradi huu umekwisha kufikia karibu miaka miwili, hivyo mradi husika umebakiza mwaka mmoja wa utekelezaji.

3.4 Mradi wa Climate Change:
Mradi huu tayari umekwisha kufungwa  rasmi.  Mradi huu ulifadhiliwa na Tanzania Media Fund (TMF) kwa mwaka mmoja, na kwamba technical report na audited report zote mbili za JET zimepongezwa na TMF, hasa jinsi zilivyoandaliwa vizuri.



3.5           Uwezekano wa kupata watu nje ya JET kuandika miradi kwa malipo kidogo:
Katika harakati za kuandika miradi ili kutafuta fedha za kuendesha shughuli za JET, tumeangalia uwezekano wa kupata watu kutoka nje ya JET kuandika miradi kwa malipo kidogo. Tumefanya hivyo, na kwa kuanzia, tumeanza na mradi mpya wa kwenda TMF.

3.6           Kuwatembelea wafadhili kutafuta miradi/ Kuandika miradi mipya:
Kuhusu suala la kuwatembelea wafadhili, tumeweza kufanya mazungumzo na Ubalozi wa Uingereza, na kufanya appointments na Ubalozi wa Finland na Norway.  Tunasubiri majibu baada ya wahusika kumaliza likizo za Noel na mwaka mpya wa 2013.
Kuhusiana na kuandika miradi mipya na kuiwasilisha kwa wafadhili, kazi kubwa iliyofanyika katika kipindi kinachohusu ripoti hii, pamoja na kutekeleza na kusimamia miradi iliyopo, ilikuwa ni kuandika miradi mipya na kuiwasilisha kwa wafadhili.

Miradi iliyoandikwa ni “Training workshop on Reporting Climate Change”, “Climate Change and Media Project” ambayo imewasilishwa BHC- Ubalozi wa  Uingereza; na Mradi wa “Improved Livelihood through Sustainable Land Management and Adaptation to Climate Change Impacts in Drylands of Tanzania” ambao umewasilishwa Global Mechanism; na wa advocacy wa Reduced Emmessions from Deforestation and forest Degradation – REDD utakaowasilishwa TMF. Tumeshauriwa na TMF kuwa tuwasilishe mradi huu Aprili mwaka huu.

4.0 Marekebisho ya Katiba: Wahesimiwa wana-JET, mtakumbuka kuwa katika mkutano mkuu uliopita wa Februari 25 mwaka jana, moja ya maazimio yaliyofikiwa ni kurekebisha katiba ya sasa ya JET ili iendane na wakati.

Baada ya azimio hilo, Kamati ya utendaji ya JET ilikaa na  kuteua mjumbe wa Kamati ya utendaji, Zainabu Mwatawala (ambaye pia ni mwanasheria), kuipitia katiba ya zamani na kuleta mapendekezo, kazi ambayo aliifanya vizuri, na mapendekezo hayo yalitumwa kwa wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji, wakiwamo wanachama wote, ili kuiboresha zaidi.  
Inasikitisha sana kuwa ni mwanachama mmoja tu aliyeleta mapendekezo yake, ukiondoa wajumbe wa Kamati ya Utendaji!
Rasimu ya katiba mpya  inayopendekezwa itawasilishwa kwenye kikao hiki
kwani ni moja ya dondoo za ajenda.

5.0           Kushirikiana na wadau wengine wa mazingira (networking)
Katika kipindi hiki ambacho ripoti hii inahusika nacho, JET iliendelea kujenga uhusiano wa kikazi na wadau mbalimbali.
Mbali na kujenga uhusiano mzuri na Serikali, JET pia iliimarisha uhusiano na wadau wapya, ikiwamo GM-Global Mechanism yenye makao makuu yake Rome, Italia, katika kitengo maalumu kinachoshughulikia masuala ya majangwa.
Mdau huyu mpya yupo katika harakati za kusaidia Serikali za Afrika pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayoshughulika na masuala ya majangwa pamoja na matumizi endelevu ya rasilimali ya ardhi.
Kama nilivyoeleza kwenye muhtasari hapo juu, Mama Misitu Campaign (MMC), TANESCO na Revenue Watch Insitute inayojihusisha na uandishi wa masuala ya gesi, mafuta na madini ni wadau wetu wapya pia.

6.0           Tuzo ya Mazingira ya JET (JET Environmental Award)
Mara mbili huko nyuma – kwa miaka miwili mfululizo - JET iliweza kuwatuza waandishi bora wa mazingira, na kukwama baadaye baada ya kukosa fedha za kuendeleza zoezi hili, hususan baada ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) kukwamisha zoezi hili baada ya kuahidi fedha na kushindwa kuzitoa.
Baadaye MCT ililidaka wazo hilo, na sisi JET tukawa watazamaji bila kuhusishwa kikamilifu katika uteuzi wa mwisho wa mshindi wa mazingira.
Kamati ya Utendaji tayari imependekeza kuwa JET irudishe Tuzo ya Mazingira ya JET kwa sababu JET ni taasisi ya mazingira, na kwamba hiyo ni ajenda yake, lakini wakati huo huo tuendelee na ushirikiano (partnership) na MCT.

Sasa mikakati na mpango kazi vinafanywa na Kamati ya Utendaji ya JET kwa kuratibiwa na wajumbe wawili wa Kamati hiyo, Dk. Ellen Otaru na Gerald Kitabu, ili kufanikisha zoezi hili.  Mikakati ni pamoja na kutengeneza documentary fupi ya mafanikio ya JET tangu kuasisiwa kwake (successs story) na kuwekwa kwenye mfumo bora ambako inaweza kuuzwa kirahisi kwa wafadhili watakaochaguliwa/kuteuliwa kwa makini.
 Orodha ya wafadhili hao inaandaliwa na italetwa kwenye kikao kijacho cha Kamati ya Utendaji kwa ajili ya kuhakikiwa na kuanza kufanyiwa kazi.

7.0 Kuhamasisha waandishi zaidi kujiunga na JET
Tangu kufanyika kwa mkutano mkuu mwaka jana Februari 25, wanachama wapya 37 wamejiunga na JET. JET pia inaendelea kuhamasisha wanachama wengine wajiunge, na inaendelea kupokea maombi mapya. Kamati ya Utendaji ya JET hukaa na kupitia maombi hayo na kupitishwa kama yakikidhi vigezo. Wanachama wapya 13 wamepitishwa na Kamati ya Utendaji kuwa wanachama mwezi uliopita (Februari 9, 20013).

7.1 Hali ya michango (ada) ya wanachama ya JET
Mojawapo ya jukumu la wanachama kwa JET ni kuhakikisha kuwa wanalipa michango yao kwa wakati ili kukipa kani (nguvu) chama chao. Kama ambavyo tumekuwa tukiwataarifu kwenye taarifa ambazo Katibu Mkuu amekuwa akiwaletea mara kwa mara, baadhi yetu hatutimizi wajibu wetu ipasavyo kwa JET.

Waheshimiwa wana-JET, kama mnavyojua, wafadhili wengi hutumia kigezo cha ulipaji ada kama mojawapo ya vigezo katika kufadhili miradi inayowasilishwa kwao.


Kwa kweli hali ya michango inasikitisha. Miongoni mwa wanachama wote wa JET wenye ithibati, kwa maana ya kuwa wanachama wa zamani, ni wanachama 26 tu ambao wametimiza majukumu yao kwa JET kwa kulipa michango yao kwa wakati. Wana-JET waliobaki wanadaiwa michango yao, na wana-JET 28 wamekwisha kufa kichama kwa kutimiza au kuzidi miaka miwili bila kulipa ada zao.

Kwa maana hiyo hawa si wanachama tena na wataondolewa kwenye orodha ya wana-JET! Katiba ya JET iko wazi.  Inasema kuwa mwanachama anakufa kichama akilaza michango yake kwa muda wa miaka miwili mfululizo. Wanachama ambao wamekufa kichama, wanaruhusiwa kuomba uanachama upya.

Katika hali hii, sekretariati ya JET inawaomba wote mtoe michango yenu ili mkipe nguvu chama chenu kipate urahisi wa kutekeleza majukumu yake, ukiwamo kuupa uanachama wenu uhai kikatiba, hasa wale ambao wako pembezoni kufa kichama.

8.0 Kiwanja cha JET

Kiwanja ambacho JET ilikuwa inafuatilia maeneo ya Mbweni JKT mwaka jana, mwenye kiwanja hicho aliendelea kutaka bei kubwa. Hivyo JET iliamua kufuatilia kiwanja kingine wilayani Kibaha ambako nako viwanja vingi tayari vilikuwa vimekwisha kuuzwa. Eneo lililokuwa limebaki ni viwanja vilivyo eneo la Jisunala, Mlandizi ambako maeneo yaliyotengwa ni kwa ajili ya shule na hospitali; na sehemu iliyokuwa imebaki kwa ajili ya ofisi ni ndogo mno, yaani sq m 4,500, ambayo pia iko umbali wa kilomita yapata 10 kutoka barabara ya Morogoro. JET haijakata tamaa, inaendelea na juhudi za kutafuta kiwanja kitakachokidhi mahitaji ya JET ya baadaye. Uharaka wa kukipata pia utategemea upatikanaji wa fedha kwa ajili ya shughuli hiyo.

9.0           Changamoto

9.1      Katika kipindi cha mwaka mmoja, kama ilivyokuwa miaka ya nyuma, mojawapo ya changamoto kubwa ilikuwa upatikanaji wa wanachama wa kutekeleza kazi mbalimbali kukidhi matakwa na viwango mahususi vya wafadhili. Hatutaki kutoa lawama kwa yeyote kwani wanachama wengi wameajiriwa na vyombo mbalimbali vya habari, na hivyo kuwajibika kwanza kwa waajiri wao.

Hata hivyo, baadhi ya wale waliopewa kazi, ama walichelewa kuzifanya, au wamezifanya chini ya kiwango au wengine hawakufanya kabisa! Hali hii imetupa kazi kweli na ugumu wa kuripoti kwa waliotoa fedha za kazi hizo, na mwisho wa siku kubomoa sifa ya JET machoni mwa wafadhili hao!
Kwa hali hiyo, tunawaomba sana wale ambao tutatakiwa kufanya kazi za chama, tuwe tayari kuzifanya kwa ufanisi mkubwa.

9.2      Kuna baadhi ya wafadhili ambao huchelewa kutoa fedha, hivyo kuathiri utekelezaji wa shughuli za miradi na kuifanya JET kuwa na wakati mgumu kuandika ripoti za miradi hiyo katika muda uliobana.

9.3      Changamoto nyingine ni mawasiliano kati ya wanachama na uongozi. Uongozi umekuwa ukiwasiliana na wanachama kwa kuwajuza yanayojiri JET mara kwa mara. Lakini mrejesho kutoka kwa wanachama umeendelea kuwa haba hasa!

Mfano mzuri ni agizo lililotolewa na wanachama kwa uongozi wa JET katika mkutano mkuu wa chama uliopita kuhusu mabadiliko ya katiba mpya. Mapendekezo ya mabadiliko hayo yalifanywa na uongozi wa JET na kutumwa kwa wanachama wote kwa ajili ya kuchangia. Ni mwanachama mmoja tu aliyeleta mrejesho, tena baada ya kutoa kumbusho!

Katika hali kama hiyo, wakati mwingine uongozi unashindwa kujua kama taarifa zilifika kwa wanachama au vinginevyo! Waheshimiwa wana-JET, inatosha tu kutuambia “asante kwa taarifa”, angalau tukajua kuwa ujumbe umefika kama wachache wenu, wachache kwa maana ya kuwa wachache, wanavyofanya.

9.4 Uandikaji na ufadhili wa miradi: Uandikaji na ufadhili wa miradi ni kazi ngumu kufanikisha, hususan linapokuja kumpata mtu kufadhili miradi hiyo. Kuandika miradi kunahitaji uweledi katika eneo hilo, na pia kuuza miradi iliyotayarishwa kunahitaji mkakati yakinifu na diplomasia isiyo haba.


10.0      Ofisi mpya za JET
Mtakumbuka kuwa tuliwaletea taarifa ya ofisi za JET kuhamia Tegeta kutoka Mnazi Mmoja katikati ya jiji. Hivi sasa ofisi hizo zipo Tegeta, Barabara ya Chanika yapata mita takriban 200 kutoka Barabara iendayo Bagamoyo. Barabara hii ipo baada ya kupita Kibo Commercial Complex upande wa kulia kama unaelekea mjini Bagamoyo.

Ilikuwaje tukahama? Mwenye nyumba ambako ofisi za JET zilipokuwa kwa zaidi ya miaka 20 alitaka kuhamia mwenyewe kwenye ofisi hizo baada ya yeye kuambiwa  pia ahame kwenye ofisi alizokuwa anapanga.

JET ilijaribu kutafuta ofisi nyingine katikati ya jiji haikufanikiwa. Ofisi nyingine zilizopatikana maeneo ya Makumbusho na Sinza, ama zilikuwa ghali sana kiasi kwamba JET tusingeweza kumudu gharama zake au zilikuwa chini ya kiwango. Ofisi za Tegeta ni nafuu na zinaridhisha. Tayari Kamati ya Utendaji ya JET imekwisha kufanyia mkutano wake mmoja kwenye ofisi hizo mpya.

11.0      Mwelekeo wa Chama kwa mwaka 2013

Mbali na kuendelea na kazi ya kuimarisha uwezo wa chama kiutendaji (capacity building), pamoja na kufanya kazi kwa uwazi kama ambavyo JET imekuwa ikifanya, shughuli kubwa zinazotarajiwa kufanywa mwaka huu ni:

·        Kusimamia utekelezaji wa miradi mipya na ya zamani, ukiwamo wa Fredskorpset, MMC na ule unaofadhiliwa na Foundation for Civil Society (FCS).
·        Kuandaa na kuandika miradi mipya
·        Kuandaa safari za kikazi (field trips)  nne  za mikoani na kuandika makala za viwango
·        Kusimamia utoaji wa gazeti la Kasuku na JET News  (baada ya kupata ufadhili)
·        Kuandaa press conferences katika maadhimisho ya Siku ya Maji Duniani, Siku ya Mazingira Duniani na Siku ya Makazi Duniani
·        Kuhamasisha wanachama kulipa michango yao kwa wakati; na kuwahamasisha waandishi zaidi kujiunga na JET


12.0 Bajeti ya JET kwa mwaka 2013
12.1  JET imekuwa ikiendesha shughuli zake kwa kutegemea vyanzo mbalimbali vya mapato. 
Mapato hayo hutokana na michango ya wanachama wake, fedha kutoka kwa wahisani mbalimbali; na fedha zitokanazo na utekelezaji wa miradi mbalimbali.
Mwanzoni mwa mwaka 2012, Bajeti iliyopitishwa ilikuwa kama ifuatavyo:
·        Mapato                                             Sh       257,107,960.00
·        Matumizi                                         Sh       253,243,488.69
·        Baki                                                  Sh             3,864,471.31

Kwa sababu baki la mapato baada ya matumizi ilikuwa ni Sh 3,864,471.31 tu, Kamati ya Utendaji iliagiza kwamba bajeti iendane na makadirio ya mapato na kufuata matumizi kama kasma zinavyoonesha. Aidha, Kamati hiyo ilipitisha mapendekezo ya Bajeti baada ya kuifanyia marekebisho.

12.2 Mwendo wa bajeti  hadi Desemba 2012
Kwa ujumla mwenendo wa bajeti katika kipindi chote cha mwaka (2012) ulikuwa ni wa kuridhisha. Pamoja na kwamba matumizi hayakuzidi mapato, matumizi ya baadhi ya miradi mbalimbali yaliweza kugharimiwa kutokana na mapato hayo hayo yaliyotokana na miradi iliyofadhiliwa.

12.3 Bajeti ya 2013
a)      Mapato
Fredskorpset:     
Kufika Desemba 31 mwaka huu (2013), tunatarajia kasma hii kuingiza kiasi cha  Sh 165,387,200.  Hili ni eneo ambalo linatuletea mapato ya uhakika, na ni mradi ambao unachangia zaidi ya asilimia 80 ya pato la chama.
Foundation for Civil Society:   
Mapato katika kasma hii yanatarajiwa kuwa Sh 52,618,000.
Mama Misitu Campaign:
Mapato katika kasma hii yanatarajiwa kuwa kiasi cha Sh 65,998,000.

Michango kutoka kwa wanachama:
Mapato yatokanayo na kasma hii, wanachama wakitoa michango yao kwa wakati, yanaweza kufikia Sh. 6,000,000.
Hivyo kwa ujumla, mapato ambayo tunatarajia kukusanya mpaka mwisho wa mwaka ujao wa fedha, ambao ni Desemba 31 mwaka huu (2013) ni jumla ya fedha za Kitanzania Sh 290,003,200 kwa mchanganuo ufuatao:
-       Sh 284,003,200 kutokana na miradi; na
-       Sh 6,000,000 yakiwa makusanyo ya michango ya wanachama wetu.
-      Mradi wa Fredskorpset utaleta kiasi cha Sh 165,387,200 (USD 103,367). Tunatarajia kubana matumizi ya Sh 48,000,000 (USD 30,000) ambazo zinaingizwa katika kasma za matumizi ya ofisi, hivyo kubakiwa na Sh 117,387,200 (USD 73,367) kwa ajili ya kuendesha shughuli za mradi mpaka mwisho wa mwaka huu wa 2013.
-      Foundation for Civil Society: Katika mradi huu tunatarajia kupata kiasi cha Sh 52,618,000 kwa kipindi cha mwaka mzima; lakini tumetengewa fedha za kuendesha ofisi kiasi cha Sh 10,478,000; hivyo kubakiwa na kiasi cha Sh 42,140,000 kwa ajili ya kuendesha shughuli nyingine za mradi kama inavyoainishwa na mchanganuo wa mapato na matumizi.

-  Mama Misitu Campaign: Katika mradi huu  tunatarajia kupata kiasi cha Sh 65,998,000 kwa kipindi cha mwaka mmoja, lakini fedha kiasi cha Sh 19,678,400 zimetengwa kuendesha gharama za ofisi, hivyo kubakiwa na Sh 46,319,600 kwa ajili ya kuendesha shughuli nyingine za mradi kama inavyooneshwa katika mchanganuo wa mapato na matumizi.
Kwa msingi huo, tunatarajia kupata jumla ya Sh 84,156,400 kama fedha za kuendesha shughuli za ofisi kutoka katika kasma tofauti kama ifuatavyo:
·        Sh 48,000,000                    kutoka Fredskorpset
·        Sh 10,478,000                    kutoka Foundation for Civil Society
·        Sh    6,000,000                   kutoka kwa Michango ya ada ya  wanachama
·        Sh  19,678,400                   kutoka Mama Misitu Campaign
Maelezo ya kina kuhusu suala hili yatafafanuliwa na idara ya Uhasibu/Mkurugenzi.

13.0  Hitimisho
Waheshimiwa wana-JET,  naomba mniruhusu nichukue nafasi hii, kwa niaba ya uongozi wa JET, niwashukuru sana wale wanachama wachache walioitikia wito wetu wa kujenga tabia ya kupitapita JET kabla ofisi hazijahama kutoka mjini ili kujionea jinsi chama chenu kilivyokuwa kinaendelea, matatizo yaliyokuwa yanakisibu na kutoa ushauri, ukiwamo wa namna ya kutafuta fedha (fund raising) kwa ajili ya kuendesha shughuli za JET.

Na wale ambao hawakupita, nao si vibaya nikiwashukuru kwa kututakia mema katika shughuli za chama chenu. Basi mwaka huu jenga tabia ya kupitapita mara kwa mara JET ili muipe sekretariati nguvu ya kusukuma mbele chama kwa kasi zaidi.

Nawashukuru sana tena, na naomba kuwasilisha.


                                   
                                  Chrysostom Rweyemamu
                                             Katibu Mkuu - JET
                                   Machi 2, 2013
                                   

Tanbihi:
Viambatanisho
1.        (Annex I) kinaonyesha mpango kazi (work plan) wa JET kwa mwaka 2003
2.        (Annex II) Rasimu ya bajeti ya fedha ya JET 2013



No comments:

Post a Comment