MDAU POPOTE ULIPO TUMA PICHA NA HABARI KWA E-mail:  antonysiame74@yahoo.com

Tuesday, April 14, 2015

Mikutano ya Majira Kipupwe imeanza rasmi Mjini Washington DC.





Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi  Philippe Dongier,  akipata maelezo kutoka kwa  Said Ngosha Magonya, ambaye ni  Kamishina wa Fedha za Nje kuhusu utaratibu uliopangwa na Tanzania katika Mikutano hii ya majira ya kipupwe.



 Mikutano ya majira ya  Kipupwe imeanza rasmi tarehe 14/4/2015 na kuhudhuriwa na nchi mbalimbali wanachama zaidi ya 188. Mikutano hii huudhuriwa na maelfu ya wafanyakazi kutoka serikalini, waandishi wa habari, Mashirika na Taasisi zisizo za kiserikali, Sekta binafsi pamoja na kamati za kifedha.Taasisi hizo kwa pamoja zitajadili maendeleo ya kazi za Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa. 

Tanzania ni nchi wanachama katika Mikutano hiyo.Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya  ndiye kiongozi wa ujumbe kutoka Tanzania na ni Gavana katika mikutano hii, akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile ambaye ni  Gavana msaidizi kwa upande wa Benki ya Dunia (WB), aidha  Gavana wa Benki kuu Prof. Benno Ndulu ni Gavana msaidizi kwa upande wa Shirika la Fedha la Kimataifa(IMF).
Hali ya hewa mjini hapa ni baridi na manyunyu ya hapa na pale.

No comments:

Post a Comment