HOTUBA
YA KAIMU MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (UVCCM), NDUGU
BENNO MALISA KWA MAKATIBU WA VIJANA WA WILAYA ZOTE NCHINI, DODOMA, 15 JANUARI
2012
Mh
Katibu Mkuu wa CCM
Mh
Katibu mkuu wa Uvccm
Mh Naibu
katibu mkuu Uvccm Znz
Mh wakuu
wa Idara makao makuu Uvccm
Mh
Mwenyekiti Mwenyeji
Waheshimiwa
Makatibu wa Uvccm Mikoa na wilaya
Waheshimiwa
Watendaji wa Chama wa Mkoani Dodoma
Waheshimiwa watoa mada,Wageni waalikwa Mabibi
na Mabwana
Kwanza niwashukuru kwa kuitikia wito wetu ikiwa ni utekelezaji
wa maazimio ya Vikao vyetu pamoja na Vya Chama ikitutaka tuwe na semina ya
namna hii kabla ya uchaguzi mkuu wa Jumuiya na Chama.
Tumekua
jumuiya ya kwanza kutekeleza agizo la chama kwahiyo hatuna Budi kujipongeza.
Pili
tumshukuru mwenyezi mungu kwa kuweza kuoona mwaka mpya na kutufikisha sote
salama hapa Dodoma
pamoja niwatakie heri ya mwaka mpya .
Napenda
kuwakaribisha vijana wenzangu na viongozi wote wa Wakati nikitoa shukrani zangu
hizo, napenda kutumia fursa hii kuwapa pole nyingi sana vijana wenzetu wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutokana na kifo cha ghafla kilichotokana
na ajali ya gari kilichomkuta kijana mwenzetu, Mbunge wa Viti Maalum, Regia
Mtema. Tunaomba Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu pema peponi.
Malengo ya
semina hii ni kama alivoeleza katibu
mkuu hapo awali kuwa ni kukutana na watendaji ,kuweka mkakati wa pamoja wa
uchaguzi wa jumuiya na chama kujadili ratiba,kanuni na utaratibu mzima wa
uchaguzi mwaka huu.
Wakati huo
huo tutajadili uchumi jumuiya,changamoto zinazotukabili vijana,hali ya
watendaji wetu na maslahi yao kwa ujumla,Vile vile kupitia kikao hiki tutatoka
na maazimio ambayo tutawekeana muda maalum juu ya utekelezaji wake.
Ndugu zangu, tunakutana leo hapa Dodoma wakati taifa na
jumuiya yetu ya vijana vikipita katika kipindi ambacho vikikabiliwa na
changamoto nyingi pengine kuliko ilivyopata kuwa wakati mwingine wowote.
Katika ngazi ya kitaifa changamoto hizo zimesababisha
kuibuka kwa kila aina ya majina yanayojaribu kueleza au kufafanua mahali ambako
kama taifa tumefikia kuwapo sasa.
Wako ambao wanasema taifa liko njia panda huku wengine
kwa sababu tu ya kujawa na hofu wamefikia hatua ya kuielezea hali tuliyomo leo
kama kipimo cha kutoweka kwa matumaini ya kitaifa au hata kukatisha tamaa.
Ndani ya jumuiya yetu, mitazamo imekuwa ni hiyo hiyo ya
baadhi yetu na hata wale walio nje kufikia hatua ya kutuona kuwa watu
tuliopoteza mwelekeo, tuliosambaratika, tuliopoteza matumaini na/au watu ambao
tumepoteza dira ya kuendelea kuwapo kwetu kama moja ya jumuiya za chama iliyo
na nguvu na ushawishi mkubwa.
Tutakuwa ni watu wa hovyo na viongozi wa ajabu iwapo sisi
wenyewe tutajifanya eti kuzipuuza hofu za namna hii zinazoelekezwa kwa taifa
letu na hata kwetu sisi tuliopewa dhamana ya kuiongoza jumuiya yetu wakati huu.
Tunayo sababu kubwa moja ya kutozipuuza hata kidogo
changamoto mbalimbali zinazowajengea Watanzania wenzetu hofu za namna hii, nayo
si nyingine zaidi ya ukweli kwamba, sisi ndiyo vijana tunaotokana na chama
kilichokabidhiwa na wananchi dhamana ya kuliongoza taifa hili.
Tukiwa kundi kubwa zaidi la kijamii ndani ya chama na
hata katika taifa kwa ujumla, sambamba na kutambua kwetu kwamba katika rika
letu sisi ndiyo nguvu kazi kubwa zaidi kuliko ilivyo kwa kundi jingine lolote,
tunapaswa kujiona na kutambua kwamba, tunayo dhamana kubwa kwa chama chetu,
serikali na kwa taifa kubwa.
Dhamana ninayozungumzia hapa si nyingine, bali ni ile
inayotupasa kuwa na majibu, tena majibu sahihi na makini yatakayotoa mwelekeo na
kumaliza kila aina ya hofu wanazokabiliana nazo wana CCM na Watanzania kwa
ujumla.
Dhamana tuliyonayo ni ile ya kuhakikisha tunakuwa mstari
wa mbele kulinda, kusimamia na kuendeleza mafanikio ya kihistoria, kimaadili na
kimaendeleo ya taifa letu ambayo tumeyapata katika kipindi chote cha miaka 50
ya Uhuru wa Tanzania Bara na 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Si hayo tu, dhamana nyingine tuliyonayo tukiwa vijana ni
kuhakikisha sisi wenyewe tunakuwa chachu ya kuhakikisha viongozi wa kisiasa na
kiserikali wanaotokana na chama chetu wanazingatia na kuheshimu maadili ya
msingi ya kiuongozi ya CCM wakati wote wanapotimiza wajibu wao.
Ni wazi kwamba ili tuweze kutimiza ipasavyo wajibu huo,
sisi wenyewe vijana tunapaswa kuthibitisha pasi na shaka kwamba malezi na
makuzi ya kisiasa, kiuongozi na kimaadili ndiyo yanayotupa jeuri mamlaka ya
kusema au kufanya kile tunachokifanya kwa bidii na kwa kujiamini.
Tutakuwa tukijidanganya wenyewe iwapo tutakuwa na fikra
kwamba tutaweza kutimiza wajibu wetu ipasavyo iwapo tutajiingiza katika vitendo
vya rushwa, matumizi ya madawa ya kulevya au katika matendo mengine yoyote
yanayoweza kutupotezea uhalali wa kiuongozi.
Ndugu zangu wakati tunapokutana leo, sisi viongozi wa
vijana, wale wa chama chetu na serikali kwa ujumla tunakabiliwa na shinikizo
kubwa la lawama kutoka kwa mahasimu wetu wa kisiasa, wanaharakati na kutoka
katika vyombo vya habari.
Lakini katika mazingira ambayo yumkini yanadhoofisha
mshikamano na misingi ya uwajibikaji wa pamoja katika jumuiya, ndani ya chama
na hata serikalini umeibuka utamaduni mpya na wa hovyo kabisa wa viongozi
kupakana matope, kuzushiana na kurushiana lawama hadharani na katika namna
inayoibua hali ambayo sisi kama vijana hatuna sababu ya kuogopa kuizungumzia.
Utamaduni huu ambao umetoa fursa hata kwa wapinzani wetu
kutushambulia umechukua picha ya wana CCM wenyewe kwa wenyewe na wakati
mwingine mawaziri kusutana kupitia katika vyombo vya habari na kwenye mikutano
ya hadhara kwa namna inayokiumiza zaidi chama kuliko kukijenga.
Watu wanaofanya hivyo wanapoulizwa kulikoni wamekuwa
wepesi wa kujificha nyuma ya vivuli mbalimbali vikiwamo vile vya eti kutumia
uhuru wao wa kidemokrasia wa kutoa maoni au wa kuuonyesha umma kwamba wanafanya
hivyo kwa nia safi ya kukabiliana na vitendo vya rushwa na ufisadi vilivyokithiri
miongoni mwa jamii kivulu kikubwa wanachojivalisha ni UZALENDO.
Ingawa hili halijawekwa wazi na kuchunguzwa kwa kina,
utamaduni huu wa viongozi kutumia vibaya uhuru wa kidemokrasia katika kukwepa
vikao halali katika kufikisha hoja zao umekuwa unaotuumiza zaidi kuliko
unavyotusaidia kama jumuiya na kama chama.
Hulka za namna hii ndizo ambazo leo hii zimesababisha
nyufa zilizo dhahiri ndani ya jumuiya yetu, miongoni mwa makada na viongozi wa
chama chetu na hata kati ya viongozi wa serikali kwa ujumla.
Ni jambo la bahati mbaya kwamba, hata baada ya chama
kutoa agizo lililokuwa likiwakumbusha viongozi na makada kutumia vikao
kufikisha hoja zao badala ya majukwaa mengine ya hadharani, bado utamaduni huu
umeendelea pasipo kukemewa.
Wala hatuhitaji wanazuoni kutoka nje ya chama chetu kuja
hapa leo na kutueleza madhara ambayo kama jumuiya na kama chama cha siasa
tumeyapata kutokana na makosa na udhaifu wetu wa kuendelea kuulea utamaduni huu
ambao hatuna budi kuchukua hatua za makusudi kuukemea na kuulaani kwa nguvu
zetu zote.
Uongozi ni kuonyesha njia. Kwa sababu ya kutambua athari
zinazotokana na kuendekeza kwetu utamaduni huo, mimi naona niwe kiongozi wa
kwanza kuwaasa viongozi wenzangu wa jumuiya hii yenye nguvu ya chama kuanza
kuchukua hatua za kuwakemea kwa uwazi viongozi wote ambao wataendeleza
utamaduni huo.
Wito wangu kwa viongozi wenzangu ni kulijadili hili
kwanza katika mkutano wetu huu kabla ya kutafuta namna bora ya kuja na azimio
ambalo litatuongoza katika kukemea na kulaani vitendo vya namna hii wakati
tutakapokuwa tumerejea katika maeneo yetu ya kazi.
Waswahili wanao msemo usemao; ‘wakati ukuta’ ambao una
maana kubwa moja kwamba katika lolote unalofanya unapaswa kuhakikisha
unalifanya katika majira na wakati unaopaswa.
Bado tunao muda wa kutosha wa kujipanga upya kwa nia ya
kusahihisha makosa makubwa ambayo tumeyafanya kabla ya kufanyika kwa uchaguzi
wa ndani ya chama baadaye mwaka huu na uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Tutaweza kufanya hivyo iwapo tutaukumbuka ushauri aliopata
kuutoa mwenyekiti wetu mstaafu wa CCM, mzee wetu, Benjamin Mkapa wakati
alipohutubia mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Agosti mwaka 2004.
Katika hotuba yake hiyo iliyokuwa na kichwa kisemacho ‘Ushupavu wa
Uongozi’, Mzee Mkapa aliwaasa wana CCM kuwa makina na kukinusuru chama chao
kujiingiza katika hatari ya ajenda zake kuandaliwa na vyama vya upinzani na
vyombo vya habari wakati kikijiandaa kuingia katika uchaguzi.
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu, maneno hayo ya Mzee Mkapa
yana maana sana leo kuliko ilivyokuwa miaka takriban saba iliyopita wakati alipoyatoa.
Hakuna asiyejua kwamba, leo hii viongozi wa kisiasa na
kiserikali wanaotokana na CCM ndiyo ambao tumekuwa mstari wa mbele katika
kuzibeba juu juu hoja za magazetini na zile za wapinzani wetu na kuzitumia kama
ajenda za kujijenga kwetu kisiasa.
Mwenye macho haambiwi tazama. Sina sababu ya kuzitaja
hapa hoja za wapinzani ambazo tumezishabikia na kuzikumbatia kwa gharama za
ustawi na heshima ya chama chetu katika jamii.
Hivi ni nani hajui kwamba, utamaduni huu wa kuiga na
kuyadaka pasipo kuyachuja na kupima kwa kina masuala yanayoandikwa magazetini au
yale yanayosemwa katika majukwaa na viongozi wa vyama vya upinzani ndiyo ambayo
yamekigharimu chama chetu kabla na hata wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka juzi?
Je, tutakuwa tukijitendea haki sisi wenyewe, chama chetu
na serikali yetu iwapo tutaendelea kuwa watazamaji na kukubali kuzama kwa
sababu ya kuwaacha wanaoutoboa mtumbwi tulioupanda? Jibu ni hapana. Tunapaswa
kuchukua hatua za kujisahihisha sasa
Ndg zangu zipo changamoto kubwa zinazotukabili ambazo
nilazima nizisemee hapa leo.
Ajira kwa vijana
Tatizo la ajira linaikumba dunia na Tanzania pia.
Vijana wengi wako mtaani si kwa kupenda, lakini hawana ajira. Ni vizuri sasa
watendaji wa UVCCM na chama tukaanza kuweka mkakati endelevu kubuni mbinu za
kuzalisha ajira kwa vijana wetu ambao ni zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania
wote.
Vijana hawa wasipopatiwa ajira kwa kubuniwa
mpango wa kuanzishwa kwa viwanda hawatatuelewa kamwe katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Lazima ndugu zangu tatambue ukweli kwamba katika Uchaguzi Mkuu ujao watakaoamua
nani au chama gani kichukue dola ni vijana maana watakuwa zaidi ya asilimia 50
ya wapigakura wote.
Ndio maana nawaasa viongozi wa chama, tuache malumbano ambayo haina manufaa kwa
vijana na tuanze mkakati maalum wa kumsaidia kijana wa Kitanzania. Lazima
tufike mahali tutambue kwamba hata kijana wa UVCCM kama hana ajira hawezi kuwa
mfuasi wako kwenye uchaguzi ujao na wala hawazi kuwa RAIA katika Taifa lake,
Serekali ya CCM imewapa ELIMU kuanzaia shule za msingi,sekondari na elimu ya
JUU ingawa kuna changamoto kubwa ambazo lazima zipate majibu na ufumbuzi wa
kisera na kimkati katika ELIMU ya Juu hasa swala mikopo, Sekondari has aswala
la waalimu na ,maabara na Ubora wa Elimu katika shule zetu za sekondari hasa za
KATA.
Hili halikwepeki kwakua sisi ji sehemu ya
Dunia na Tanzania,matatiuzo
haya ni yetu sote Ajira inamuathiri kila Kijana na Kijana wa CCM nae ni
muathirika tusidhani sisi si sehemu ya ,matatizo.
Ndg kwa kutambua hili ninaagiza mikoa ya
RUKWA,MBEYA,RUVUMA,IRINGA,MOROGORO,DODOMA,SINGIDA,TABORA,KIGOMA,KAGERA,MWANZA,MARA,LINDI,MTWARA,MANYARA,KASKAZINI
PEMBA,KASKAZINI UNGUJA kila wilaya kufikia mwezi wa pili mwaka huu Tarehe
15 kamati za utekelezaji zikutane na
waaalike wakuu wa wilaya,na wenyeviti wa halmashauri katika maeneo ambayo
hatuna wenyeviti wa halamshauri waalikwe wakurugenzi wa halamshauri na kujadili
uanzishwaji wa mashamba ya Uvccm na kila wilaya ipate eneo walau HEKAARI 300.
Na kwa upande wa Zanzibar
walau HEKARI 50,
Jumuiya makao makuu tutakua na jukumu la
baada ya upatikanaji wa ardhi tutafanya utaratibu wa ukopaji wa matrekata
kwakutumia hati za mashamba hayo kufikia
mwezi wa tano mwaka huu zoezi hili liwe limekamilika kitaifa.
Kupitia mashamba haya tutahakikisha yanakua
ni sehemu ya kuleta ajira kwa Vijana na sisi kuwa sehemu ya kupunguza
tatizo hilo Mfumo wa uendeshaji wa mradi
huu utaandaliwa na mimi Binafsi nitaanza ziara katika mikoa niliotaja na kupita
kila wilaya kuanzia mwezi wa Pili tarehe 25th.
UCHUMI
WA JUMUIYA.
Ndg zangu jumuiya yetu imepita katika kipindi
kigumu toka enzi za kina Guninita,Dk Emanuel Nchimbi na SASA lakini tunakila
sababu ya kumshukuru Dk Nchimbi,Uongozi wote uliopita Chini ya Baraza la
wadhamini linaloongozwa na Waziri mkuu Mstaafu Ndg Edward Ngoyai Lowasa kwa
kutusaidia kuanzishwa kwa Mradi wa Majengo PACHA ya UBIA ambayo yataifanya
Jumuiya hii kuwa ya kwanza kujitegemea kiuchumi,tulitukanwa sana na
kudhalilishwa kwa MRADI HUU na baadhi ya Viongozi wenzetu wa chama lakini leo
niwaambie ushirikiano na umoja mlionyesha kama watendaji kuanzia mwezi wa Tano
mwaka huu KUOMBA KUMEISHA TUTAKUA JUMUIYA HURU KIUCHUMI.Niwaahidi matunda haya
hayatokua ya makao makuu tu bali niyenu nyote na nyinyi mtakua miongozi mwa
watu wataokao Faidika,tutaanza kuongeza Kipato chenu mara baada ya mradi huu
kuazia kutumika mwezi june.
Niwatakle mikoa na wilaya endeleeni kubuni
miradi na kufufua miradi iliyokufa na katika mikoa niliyotaja nitakapoanza
ziara yangu kukagua utekelezaji wa mradi huu wa kilimo nintaka kujua miradi
hiyo na iliyokufa katika kila wilaya na mkoa.
Katiba Mpya
Mbali na uchaguzi wa jumuiya ndani ya chama,
uchaguzi wa chama, kuna suala muhimu sana
nalo ni mchakato wa Katiba Mpya ambao Rais wetu mpendwa, Jakaya Kikwete
aliuasisi mara baada ya kuchaguliwa kuiongoza nchi kwa mara ya pili.
Hili ni tukio la kihistoria ambao sisi kama viongozi na watendaji wa UVCCM lazima tushikane bega
kwa bega na viongozi wetu katika kuhamasisha vijana washiriki kutoa maoni kwa
ajili ya kutengenezwa kwa Katiba Mpya. Vijana wa CCM lazima tuonyesha kwamba
tuko mstari wa mbele kuhamasisha umma utoe maoni kuhusu Katiba Mpya kwa kuwa ni
jambo jema kwa manufaa ya Tanzania
ya sasa na ya zaidi ya miaka 50 ijayo.
UCHAGUZI
WA CHAMA NA JUMUIYA
Ndugu zangu vijana wenzangu, uchaguzi wa mwaka
huu ni muhimu sana
katika historia ya chama chetu, ni uchaguzi ambao unaweza kutufanya tukaimarika
zaidi mbele ya umma wa Watanzania au kutuboa mbele ya jamii hasa vijana ambao
si wanachama wetu, lakini tunawahitaji kwa dhati watuunge mkono katika chaguzi
zijazo cha Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Ndugu zangu watendaji, ni matumaini kwamba uchaguzi huu utaendelea
kujenga umoja wetu na kutuweka karibu zaidi na vijana wenzetu kama utafuata
taratibu ambazo tumejiwekea na ambazo zinakubalika na Chama chetu Cha Mapinduzi
bila kuingiliwa na watu wenye ajenda zao za siri na ambao si wanachama wa
jumuiya yetu.
Ndio maana napenda kusisitiza kwamba uchaguzi
wa jumuiya ni wanajumuiya kwa maslahi ya chama chetu. Nimeamua kusema haya ili
mkioona watu wakipita huko wakiwaambia mchagueni huyu kwasababu ni wa kundi
langu, kataeni, waambieni hapa tunachagua viongozi bora wa kuitumikia jumuiya,
chama chetu na taifa letu, hatuchagui kundi la mtu hapa kwa ajili ya maslahi
yake binafsi.
Ndio maana aliyekuwa Waziri Mkuu wa
Uingereza, Tony Blair aliwahi kunukuliwa akisema kwamba ‘’The art of leadership is
saying no, not saying yes. It is very easy to say yes, akiimanisha kwamba
kipaji cha uongozi ni uwezo wa kiongozi kusema HAPANA, na siyo kusema NDIO kwa
kuwa ni rahisi sana
kusema NDIO. Nukuu hii ya Tony Blair ni muhimu sana
katika uchaguzi ndani ya jumuiya yetu, tunataka watendaji wetu wafuate amri za
kanuni zetu ambazo tumejiwekea na si maagizo ya watu fulani ambao malengo yao
hatuyajui.
MWISHO
Mwisho
ndgzangu katika kipindi change cha uongozi na huu ukiwa ni mwaka wa mwisho
mmenipa ushirikiano mkubwa sana ambao umetuwezesha kuvuka mabonde na milima na
kwa hilo leo tuko wamoja jumiya yetu haina makundi wapo wachache wanotaka
kutuvuruga ndugu zangu mimi nipo Imara tusiwape fursa hiyo tunaelekea katika
uchaguzi niwatake vijana wote wenye uwezo na nia njema wajitokeze katika kila
nafasi ili tuwe na uwakilishi mkubwa ndani ya chama kujenga JUMUIYA MPYA NA CCM
MPYA 2012,Kauli MBIU YETU KAMA JUMUYA NI “ UVCCM MPYA KUELKEA CCM MPYA”
Sntakua
kuwa mwema nisimp mshukuru rais jakaya mrisho kikwete na viongozi wa chama
wamekua wakitupa ushiorikiano mkubwa katika kufanya shughuli zetu tunampongeza
Rais klwa kazi nzuri anayofanya anakumbana na changamoto nyingi niseme kuwa
Hayuko peke yake tuko nae na hatuyumbi
No comments:
Post a Comment