MDAU POPOTE ULIPO TUMA PICHA NA HABARI KWA E-mail:  antonysiame74@yahoo.com

Sunday, May 11, 2014

KAMPUNI ya Dar Brew maarufu zaidi kama Chibuku, imezindua rasmi bia mpya ya asili ijulikanayo kama ‘Chibuku Super’,






Kiwanda cha Dar Brew, kimezindua aina mpya ya Bia ijulikanayo kama “Chibuku Super”. Bia hii inayopatikana katika chupa nzuri naya kuvutia ya plastiki, isiyorudishwa (take away) ina ujazo wa lita moja na itauzwa kwa bei ya shilingi 1,200/- tu kwa chupa. Uzinduzi huo uliojawa na burudani zisizo kifani, ilihudhuriwa na wafanyakazi wa kiwanda hicho, wauzaji wa jumla na rejareja na wageni wengi waalikwa.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo uliofanyika katika viwanja vya kiwanda hicho kilichopo eneo la Ubungo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi mkuu wa Dar Brew Bw. Kirowi Suma alisema; Leo ni siku ya furaha kubwa sana kwetu Dar Brew na kwa watumiaji wote wa Bia, kwani tumeweza kuzindua Bia hii mpya ya “Chibuku Super” ambayo inatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika soko la Bia hapa nchini. Bia hii imetengenezwa kwa utaalam wa hali ya juu na kwa kutumia mitambo ya kisasa kabisa, hivyo kuwahakikishia wanywaji Ubora wa hali ya juu. Alisema Suma
Bw. Suma alisema, Bia hii inatengenezwa kwa kutumia malighafi za hapa nyumbani, ikiwemo nafaka ya mtama bora toka kwenye ardhi yetu, haya yote yanatupa kila sababu sisi watanzania kujivunia kilicho chetu na kukumbuka Asili yetu, kwani hii ni Bia yetu ya asili. Chibuku Super ina kilevi cha asilimia 4, kinachokufanya uweze kuitumia kwa muda mrefu ukiwa na marafiki, lakini pia inakupa lishe nzuri kutokana na virutubisho vinavyopatikana katika nafaka zinazotumika kutengeneza bia hii. Kwa sasa Bia hii itaanza kupatikana katika mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Morogoro na Dodoma, kisha itaenea nchi nzima.
Akizungumzia juu ya usambazaji wa Bia hii, meneja mauzo wa Dar Brew Bw. Saidi Mremi amesema; Baada ya uzinduzi huu unaofanyika leo, Bia hii ya Chibuku Super itaanza kupatikana kesho katika Baa zote, Super Markets, na sehemu nyinginezo zinazouza vileo. Tunatarajia wateja na wapenzi wa bia wataifurahia bia hii mpya itakayouzwa kwa bei ya shilingi 1,200/- tu kwa chupa yenye ujazo wa lita moja.
Na kwa wauzaji wa jumla, tunatarajia watahamasika kuuza bia ya Chibuku Super kwani ina faida nzuri na haina usumbufu wa kununua chupa, kwani chupa zake hazirudishwi (Take away), alisema Mremi
Tuna imani kubwa wapenzi wa Bia wataipokea bia hii mpya kwa Shangwe na furaha kubwa, na pia watatumia Bia hii kuonesha kuwa wanajali Asili yao. Alimaliza Mremi.

No comments:

Post a Comment